Pages

Monday, October 17, 2011

BAADA ya kuandamwa na ‘kashikashi’ za kisiasa kwa muda mrefu, Mbunge wa Monduli, Edward Ngoyai Lowassa (CCM), ameonekana ‘laivu’ runingani akifuatilia kwa karibu ibada ya Kiongozi Mkuu wa Huduma ya Kikristo ya Synagogue Church of All Nations (SCOAN), Mtume na Nabii Temitope Balogun Joshua ‘T.B Joshua’ huko Lagos, Nigeria.

Ishu hiyo ambayo imekuwa gumzo katika mitandao fulani fulani ilijiri hivi karibuni ambapo waziri mkuu huyo mstaafu alionekana kupitia Runinga ya Emmanuel TV.
Katika ibada hiyo iliyokuwa na ‘taito’ ya Sunday Live Service, ujumbe wa siku hiyo ulikuwa ni kushinda woga katika kujaribu kutenda jambo lolote.

T.B Joshua ni mmoja wa viongozi wenye heshima duniani aliyejipatia umaarufu kutokana na unabii anaoutoa kuhusu masuala mbalimbali, uponyaji kwa njia ya maombi na maombezi ya kawaida.
Habari kutoka Global Publishers
:) :( ;) :D ;;-) :-/ :x :P :-* =(( :-O X( :7 B-) :-S #:-S 7:) :(( :)) :| /:) =)) O:-) :-B =; :-c :)] ~X( :-h :-t 8-7 I-) 8-| L-) :-a :-$ [-( :O) 8- 2:-P (:| =P~ #-o =D7 :-SS @-) :^o :-w 7:P 2):) X_X :!! \m/ :-q :-bd ^#(^ :ar!

No comments: